Monday, May 6, 2013

RVP ANGOJEA KOMBE LA UBINGWA KWA HAMU KUBWA!!


Jumatatu, 06 Mei 2013 21:32
ChapishaToleo la kuchapisha
>>RVP: “NIMESUBIRI MUDA MREFU KUWA BINGWA!!”
>>ALIHAMA KUSAKA TAJI, SI KUPIGANIA 4 BORA MIAKA NENDA RUDI!
>>KOMBE RASMI OLD TRAFFORD JUMAPILI MEI 12!!
RVP_in_RED2ROBIN VAN PERSIE amekiri kuwa amengoja muda mrefu mno hadi kutwaa Taji lake la kwanza la Ubingwa wa BPL, Barclays Premier League, na Jumapili ijayo, ndani ya Old Trafford, wakikabidhiwa Kombe lao baada ya Mechi yao na Swansea City ambayo ndio ya mwisho Msimu huu Nyumbani kwao, itakuwa ni kutimia kwa ndoto yake.
Jumapili, Mei 12, Siku ambayo Man United watakabidhiwa Kombe la Ubingwa wa BPL, itakuwa ni Wiki 3 tangu Robin van Persie apige Hetitriki walipoifunga Aston Villa 3-0 na rasmi kuwatazwa kuwa Mabingwa.
Ushindi huo na Bao hizo za Van Persie ulikuwa ni uthibitisho rasmi kuwa yeye ndie alikuwa ufunguo wa Man United kutwaa Taji lao la 20 la Ubingwa na kuzidi kujikita kuwa wao ndio Klabu Bora England kwa kutwaa Mataji mengi kupita nyingine yeyote.RVP-UBNGWA_NA_20
Van Persie, ambae aliihama Arsenal mwanzoni mwa Msimu huu ili asake Mataji badala ya kupigania kufuzu 4 Bora Miaka nenda rudi, ametamka: “Ni hisia ambayo huwa unaiota tu! Kila kitu ni kunyanyua lile Kombe! Tulipigaji Picha safi tulipoifunga Villa na kutwaa Ubingwa lakini kuna kitu kilikosekana! Ni Kombe!”
Aliongeza: “Hiyo ndio Picha nitaitia fremu na kuitundika Nyumbani kwangu, mimi nikinyanyua Kombe la Barclays Premier League! Nashindwa kusubiri muda huo! ”
Wakati akihamia Man United mwanzoni mwa Msimu kuna baadhi ya Watu walikuwa na wasiwasi na uhamisho huo lakini kwa Sir Alex Ferguson, Meneja wa Man United, na Van Persie, kulikuwa hamna hilo na mwenyewe Van Persie anaeleza: “Nisingehama kama ningekuwa na mashaka. Tangu Siku ya kwanza nilikuwa nina hakika tutashinda Msimu huu. Niliona Wachezaji mazoezini. Niliwaona wanavyojituma, wao na Makocha. Ukichanganya vyote hivyo unapata Timu ya Mabingwa. Kubwa zaidi ni kuwa pamoja na Timu yenye Wachezaji wanaojua kushinda.”
Mbali ya Kombe la Ubingwa, Van Persie pia ndie anatarajiwa kutwaa Butu ya Dhahabu kwa kuwa anaongoza akiwa Mfungaji Bora wa BPL akiwa na Goli 25 na kufuatiwa na Luis Suarez wa Liverpool, ambae yupo Kifungoni Mechi 10 hivyo hatamletea upinzani, na anaefuatia ni Gareth Bale ambae yuko Bao 5 nyuma.
Lakini mwenyewe Van Persie anasema: “Ukweli ni kuwa hiyo Tuzo si sahihi. Haya Magoli ni ya Timu nzima. Bora wangetoa Kiatu cha Dhahabu kwa Timu! Ingawa itafurahisha kushinda hiyo lakini Ubingwa ndio muhimu!”
WAFUNGAJI BORA:
NA
JINA
TIMU
GOLI
1
Van Persie
Man United
25
2
Suarez
Liverpool
23
3
Bale
Tottenham
20
4
Benteke
Aston Villa
18
5
Michu
Swansea
17
6
Ba
Chelsea
15
7
Lambert
Southampton
14

Lukaku
West Brom
14
8
Berbatov
Fulham
13

Lampard
Chelsea
13

Walcott
Arsenal
13
9
Cazorla
Arsenal
12

Dzeko
Man City
12

Rooney
Man Utd
12
10
Aguero
Man City
11

Defoe
Tottenham
11

Fellaini
Everton
11

Fletcher
Sunderland
11

Giroud
Arsenal
11

Kone
Wigan
11

Le Fondre
Reading
11

Tevez
Man City
11
BPL, BARCLAYS PREMIER LEAGUE
RATIBA
Jumatatu Mei 6
[Saa 4 Usiku]
Sunderland v Stoke
Jumanne Mei 7
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Man City v West Brom
Wigan v Swansea
Jumatano Mei 8
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Chelsea v Tottenham
Jumamosi Mei 11
[Saa 8 Dak 45 Mchana]
Aston Villa v Chelsea
Jumapili Mei 12
[Saa 9 na Nusu Mchana]
Stoke v Tottenham
[Saa 11 Jioni]
Everton v West Ham
Fulham v Liverpool
Norwich v West Brom
QPR v Newcastle
Sunderland v Southampton
[Saa 12 Jioni]
Man United v Swansea
Jumanne Mei 14
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Arsenal v Wigan
[Saa 4 Usiku]
Reading v Man City
Jumapili 19 Mei
***MECHI ZA MWISHO ZA LIGI MSIMU HUU
[Saa 12 Jioni]
Chelsea v Everton
Liverpool v QPR
Man City v Norwich
Newcastle v Arsenal
Southampton v Stoke
Swansea v Fulham
Tottenham v Sunderland
West Brom v Man United
West Ham v Reading
Wigan v Aston Villa
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO:
**FAHAMU: BINGWA TAYARI NI MANCHESTER UNITED!!
NA
TIMU
P
GD
PTS
1
Man Utd
36
42
85
2
Man City
35
30
72
3
Chelsea
35
34
68
4
Arsenal
36
31
67
5
Tottenham
35
18
65
6
Everton
36
14
60
7
Liverpool
36
25
55
8
West Brom
35
1
48
9
Swansea
35
-1
43
10
West Ham
36
-8
43
11
Stoke
35
-10
40
12
Fulham
36
-11
40
13
Aston Villa
36
-21
40
14
Southampton
36
-11
39
15
Norwich
36
-22
38
16
Newcastle
36
-23
38
17
Sunderland
35
-12
37
18
Wigan
35
-22
35
19
Reading
36
-26
28
20
QPR
37
-29
25
**QPR & READING TAYARI ZIMESHUKA DARAJA

No comments:

Post a Comment